UGONIWA WA KISUKARI NA SARATANI
Tafiti zinaonyesha kwamba kuna wakati saratani ni matokeo ya
mchakato wa ukarabati wa seli zilizoharibika ndani ya mwili. Tafiti hizi
zinaonyesha kwamba mimba inapotungwa seli katika mimba hiyo changa hugawanyika
haraka sana na kutengeneza makundi mawili ya seli zenye maumbile na kazi
tofauti. Kundi la kwanza la seli hizo (Kiini tete, au embryo kwa lugha ya
kitaalamu) huendelea kugawanyika na
kubadilika likiwa safari kutengeneza kiumbe ambacho hatimaye kitazaliwa
kama mtoto. Hali kadhalika kundi la pili nalo hundelea kugawanyika na
kubadilika na hatimaye kutengeneza kondo la uzazi (placenta) ambalo kazi yake
ni kulizingira lile kundi la kwanza.
Kila moja ya seli katika kundi hili la seli ambalo sasa
limetengeneza kondo la uzazi ina gamba ambalo limebeba umeme hasi. Seli hizi
kitaalamu huitwa Trophoblasts. Kazi ya
hizi Trophoblasts ni kutoa ulinzi kwa kiini tete kisiweze kushambuliwa na mfumo
wa kinga za mwili za mama! Bila seli hizi chembechembe nyeupe za damu katika
mwili wa mama ambazo huunda sehemu kubwa ya jeshi la kinga katika mwili wa
mwanadamu zingeshambulia kiini tete hicho na kukiharibu kwa dhana kwamba ni
adui ailiyeingia mwilini! Kinachotokea ni kwamba kwa kuwa chembechembe hizi
nyeupe za damu nazo zimebeba umeme hasi kama zilivyo Trophoblasts,
zinapokaribia eneo kiliko kiini tete umeme hasi wa Trophoblasts na ule wa
chembechembe cheupe husukumana (repels each other) na hivyo kusababisha
chembechembe hizo nyeupe kusogezwa mbali na kiini tete. Tafiti zinaonyesha kuwa
ulinzi huu wa Trophoblasts hukoma ghafla katika juma la nane la ujauzito.
Tafiti zinaonyesha kuwa sababu ya hatua hii ni kwamba katika
kipindi hiki kiumbe kinachoendelea kukua na kubadilika tayari kina ngongosho
linalofanya kazi na kongosho hili huzalisha kiasi kikubwa cha vimeng’anyo
(pancreatic enzymes) ambavyo haviruhusu trphoblasts au chembechembe nyeupe za
damu kutoka kwa mama kusogea katika eneo hilo. Vimeng’enya hivi vina uwezo wa
kuchakatua na kuyeyusha protini (digest) hivyo basi chembechembe yoyote nyeupe
katika eneo hilo, au seli ya trophoblast itaharibiwa kwa protini yake
kuchakatuliwa na kuyeyushwa na vimeng’enya hivyo.
Tafiti zinaonyesha kuwa mwili unapositisha uzalishaji wa
trophoblasts, chache ya hizi seli hubakia zikiogelea kwenye damu katika kipindi
chote cha maisha ya kiumbe. Kazi ya hizi trphoblasts ni kusaidia katika
ukarabati wa seli za mwili zinazoharibika kwa sababu mbalimbali. Katika eneo
ambalo seli zimeharibika na zinahitaji kukarabatiwa seli chache za trophoblasts
huenda katika eneo hilo na kuanza kugawanyika kwa kasi inayozifanya kuongezeka
kwa wingi ndani ya muda mfupi, huku zikifanya kazi ya kusadia ukarabati. Tatizo
linakuja pale ambapo uharibifu wa seli husika ni kitendo endelevu na pengine
cha kudumu. Kwa mfano, kwa wavutaji wa sigara wa muda mrefu ambapo uharibifu wa
seli za mapafu yao ni endelevu. Hii ina maana kwamba katika eneo husika
trophoblasts zitakuwa zinajigawanya kwa kasi na zitaongezeka kupindukia mipaka
(out of control growth).
Uchunguzi wa kimaabara unaonyesha kuwa seli za trophoblasts
zinazojikuta katika mazingira ya aina hii hufanana kwa kila hali na seli za
saratani! Hii imepelekea baadhi ya wanasayansi kuamini kuwa saratani chanzo
chake ni nia nzuri na jitihada ya mwili kutaka kurekebisho kasoro
zinazojitokeza katika seli za mwili. Jitihada zinapokwenda mrama kutokana na
uharibifu katika seli husika kuwa endelevu basi saratani hujitokeza. Imethibitika
kuwa vimeng’enyo vinavyozalishwa na kongosho (pancreatic enzymes) ni msaada
mkubwa wa kuzuia trophoblasts kutengeneza saratani mwilini.
Ugunduzi huu ulifuatia jitihada kubwa za Dr. William D.
Kelly wa kule nchini Marekani ambaye aliamini kuwa saratani ni zao la mwili
kushindwa kuchakatua vizuri vyakula vya jamii ya protini kutokana na upungufu
wa vimeng’enya vinavyozalishwa na kongosho, hususan vile ambavyo kazi yake ni
kuchakatua na kuyeyusha protini (proteolitic enzymes).
Ili kuusadia mwili kufanya kazi hiyo kwa ufanisi Dr. Kelly
alipendekeza mfumo wa tiba kwa wagonjwa wake ambao ulijumuisha marekebisho
katika lishe, matumizi ya tiba-lishe (nutritional suppliments), na uondoshaji
wa sumu mwilini. Dr. Kelly ambaye alipingwa sana na madaktari wa mfumo
(conventional cancer doctors) alisafishwa na Dr. Nicholas Gonzales wa Newyork
ambaye alifanya kazi kubwa ya kutafiti kesi moja moja ya wagonjwa wa Dr. Kelly
kwa udhamini wa taasisi ya Memorial Sloan - Kettering Cancer Center. Ripoti ya
kazi ya Dr. Gonzales, iliyokuwa na kurasa 500, ilithibitisha kuwa tiba ya Dr.
Kelly ilikuwa kweli inafanya kazi katika saratani za aina nyingi mwilini.
Utafiti wa ziada uliofanywa katika kazi ya Dr. Kelly na
wengine waliomfuata umethibitisha bila shaka kuwa uchache wa vimeng’enya vya
kongosho ni sababu ya msingi ya kuibuka kwa saratani mwilini; na kuwa wagonjwa
wa ugonjwa wa kisukari ambao kimsingi kongosho zao zinazalisha kiwango kidogo
cha hivi vimeng’enya, wako katika hatari mara tatu zaidi ya kupata ugonjwa wa saratani.
Hii ina maana kuwa mgonjwa wa kisukari anatakiwa achukue
tahadhari mara tatu zaidi kuliko mtu wa kawaida katika kulinda seli zake za
mwili zisiharibike na kujenga mazingira ya trophoblasts kuzaliana kwa wingi.
Uharibifu huu ni ule unaoweza kufanywa na uvutaji wa sigara, ulaji wa vyakula
vilivyotunzwa kwa kemikali, matumizi ya vipodozi bandia (synthetic cosmetics),
matumizi ya nyama zilizochakatuliwa na kuhifadhiwa kwa kemikali, matumizi ya
nyama za kuchoma zilizoungulia na kufanya mkaa, nakadhalika. Aidha mgonjwa wa
sukari anahitaji kutumia nyongeza/tiba- lishe (nutritional supplements) za
vimeng’enya, hususan vile ambavyo kazi yake kubwa ni kuchakatua na kuyeyusha
protini.







No comments:
Post a Comment