Tuesday, June 14, 2016

KISUKARI CHA UKUBWANI NI RAHISI KUTIBIKA – ELEKEZA JITIHADA KATIKA KUDHIBITI MFURO (INFLAMMATION)




Mfuro ni kitu gani?

Umeshawahi kujikwaa ukiwa hukuvaa viatu? Au umeshawahi kujigonga/kugongwa kwa nguvu kidogo, hasa kichwani au kwenywe paji la uso? Inawezekana baada ya matukio haya ulishuhudia uvimbe katika vidole vya mguu, au nundu katika kichwa au paji lako la uso. Basi huo ni mfuro.

Ukiachilia mbali mifuro inayosababishwa na kujiumiza kimwili moja kwa moja kama tulivyoeleza katika hiyo mifano hapo juu, seli zetu za mwili kuanzia za ndani hadi zile za nje huweza kupatwa na mfuro kwa sababu nyingine mbalimbali.

Kwa kawaida kinga za mwili zinapoingia kupambana na kitu chochote kile zinachikidhania ni hatari kwa mwili, moja ya matokeo katika eneo la mapambano ni mfuro. Hii ina maana kwamba kila unapopata maambukizi yoyote yale, pamoja na ugonjwa wenyewe unaosababishwa na hayo maambukizi, sehemu ya maamivu unayokabiliana nayo hutokana na kuenea kwa mfuro mwilini. 

Kwa bahati mbaya sana maisha ya kisasa yametawaliwa na vitu vingi sana vinavyosababisha kinga za mwili ziwe katika mkao wa vita muda wote.  Vitu hivi ni pamoja na baadhi ya vyakula; vinywaji ; dawa (hususan zile za kifamasia); na vipodozi. Baadhi ya vitu hivi vinapoingia ndani ya mwili huchochea kinga za mwili kudhani kuwa adui kaingia; na kwa hivyo moja kwa moja huingia katika mapambano. Kwa kuwa vitu hivi tunakutana navyo kila siku na kila mara, hii ina maana kuwa miili yetu inakabiliwa na mfuro karibu muda wote. Inaaminika kuwa miongoni mwa vyakula vinavyochochea mfuro kwa kiwango cha juu sana ni nafaka zote zilizochakatwa (kuondoa ganda la juu); sukari; na mafuta yanayotokana na mbegu pale yanapotumiwa kwa matumizi ya kupikia.  Mafuta ya mbegu ni pamoja na yale ya alizeti, ufuta, mawese, karanga, pamba, nakadhalika.

Kitu kingine kinachosababisha mfuro endelevu ni mtindo wa maisha wa kubweteka. Kiasili hatukuumbwa tuwe ni watu wa kutulia eneo moja kwa muda mrefu.  Maumbile yetu yanahitaji viungo vyetu viwe vinajongea muda mwingi pale tunapokuwa tuko macho. Tafiti zimebainisha kuwa kuketi au kujilaza sehemu moja muda mrefu (nusu saa au zaidi) kunauingiza mwili uwe katika hali ambayo inasababisha mfuro katika seli. Moja ya namna za kutambua kiwango cha mfuro mwilini ni kupima kiwango cha chembechembe zinazoitwa C- Reactive Protine (CRP). Tafiti zinaonyesha kuwa CRP inaongezeka katika mzunguko wa damu kwa kitendo cha kuketi tu sehemu moja kwa muda mrefu.

Madhara ya Mfuro.

Umeshawahi kukutana na tukio la kusumbuliwa na mlango wa mbao wakati wa kuufunga au kuufungua, hususan wakati wa msimu wa mvua? Kuna baadhi ya mbao zina tabia ya kunyonya unyevu unyevu na kufura. Milango au madirisha yanayotengenezwa na aina hii ya mbao mara nyingi inaweza ikasumbua wakati wa  kufunga au kufungua wakati wa vipindi vya mvua endelevu.  Mfano huu ni sawa na kinachotokea kwenye seli inayokabiliwa na mfuro.

Kila seli ina vitu vinavyoitwa ‘vipokezi’ au kwa kitaalamu cell receiptors. Vipokezi hivi ni sawa na milango na madirisha. Moja ya kazi ya vipokezi hivi ni kupokea viini-lishe, maji na gesi ya oxygen kutoka nje ya seli na kuviingiza ndani ya seli kwa ajili ya majukumu mbalimbali.  Kazi nyingine ni kutoa nje ya seli uchafu wa mabaki ya viini-lishe, maji yaliyotumika na hewa chafu kwa ajili ya kuondolewa mwilini. 

Vipokezi kwenye seli yenye mfuro ni sawa na mbao ya dirisha au mlango inayonyonya unyevu nyevu.  Mfuro hupelekea vipokezi hivi visifanye kazi kwa ufanisi. Wataalamu wengi wanaamini kuwa kutokana na hali ya miili yetu kukabiliwa na mfuro ambao ni endelevu, ufanisi wa vipokezi katika seli zetu uko chini sana na hali hii ndiyo chimbuko kubwa la maradhi mengi ya kimfumo, ikiwa ni pamoja na ugonjwa wa kisukari.

Chukua Hatua Kukabiliana na Mfuro

Hatua muhimu katika kukabiliana na mfuro ni pamoja na:
  1. Kuacha kula vyakula vinavyochochea mfuro. Kama ambavyo tumekwishaona, vyakula hivi ni vile  vyote vinavyotokana na nafaka zilizochakatwa. Vingine ni SUKARI na vile vilivyopikwa kwa mafuta ya mbegu, yaani vegetable oils;
  2. Kuvifanya viungo vyote vya mwili viwe katika hali ya kujongea (move) kila mara. Ni vema kutoruhusu kuketi sehemu moja kwa muda unaozidi nusu saa. Nyanyuka, jinyooshe, tembea hatua mbili tatu, kisha rejea kwenye kiti chako kila baada ya muda fulani. Mazoezi ya viungo ya walau siku nne kwa wiki ni msaada mkubwa. Hata hivyo pale ambapo fursa ya kufanya mazoezi ni finyu, ni muhimu kutenga muda kila siku na kutembea kwa mguu kiasi cha kiliometa tatu au nne;
  3. Hakikisha unajitibu magonjwa yote ya maambukizi yaliyoko mwilini mwako; na
  4. Jenga tabia ya kula au kunywa vitu vyenye sifa ya kukabiliana na mfuro. Baadhi ya vitu hivi ni pamoja na:
    1. Viungo kama manjano; tangawizi; karafuu; jira (binzari nyembamba); na habat Sauda (black seed);
    2. Chai ya kijani (green tea); na
    3. Matunda kama zabibu, zambarau


No comments:

Post a Comment